Hatimaye Ndoto Imetimia..Jack Wolper Kufunga Ndoa

8 years ago100 Views

BAADA ya kupitia misukosuko mingi katika mahusiano ya kimapenzi, malkia wa fashion na mkali wa filamu za Bongo, Jacqueline Wolper huenda akafunga ndoa hivi karibuni mara baada ya kuanika mipango yake ya kwenda kumtambulisha mpenzi wake kwa wazazi.

Japo hajataja jina, Wolper ameeleza kuwa mpenzi wake huyo ameridhia suala hilo kwani naye pia alikuwa akilihitaji toka mwanzo huku akibainisha kuwa amejifunza kunyamaza bila kuweka hadharani mahusiano yake na siku ya leo ndipo anatarajia kumtambulisha nyumbani kwao, Moshi na taratibu nyingine kama mahari kufuata.


ALICHOKIANDIKA WOLPER


Wewe ni mwanaume ambae umejitoa ili tu niwe wako, umetaka tufike mbali kwanza kabla ya mambo mengine (uwende kwa wazazi, (NDOA) pamoja na kwamba mahusiano yangu ya nyuma yalikuwa yana misukosuko mingi ila umemthamini Jacq. Nilipotoka niliteswa sana na mapenzi yaani usaliti, dharau, kukosa na mapenz ya dhati.


“Pamoja ya kuwa pia alishatokea mmakonde na kunipeleka mapaka Mtwara na matembele nikachuma na wanakijiji kunipokea na kupikia familia na kutambulishwa kwa wazazi lakini sikufanikiwa kufikia hatua hii ambayo umefika, umenijali na umenisikiliza nilipokwambia sihitaji mtu bali nahitaji future husband,” ameandika Wolper. 

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.