HATARI:Kenya Wananchi Wakatazwa Kutoka nje Jioni Hadi Alfajiri

Masama BlogKITAIFANAFASI ZA KAZI4 months ago220 Views

Kenya Wananchi Wakatazwa Kutoka nje Jioni Hadi Alfajiri

Mamlaka nchini Kenya imeweka marufuku ya kutotoka nje kwa siku saba kuanzia jioni hadi alfajiri katika baadhi ya sehemu za kaunti ya Nakuru baada ya kuanza kwa ghasia za kikabila.

Takriban mtu mmoja ameuawa na wengine wanane kujeruhiwa huku nyumba takriban 12 zikichomwa moto kufuatia mapigano ya kikabila huko Tipis na maeneo ya Mwisho wa Lami.

Vurugu hizo, ambazo ziliibuka Jumamosi katika mpaka wa Nakuru -Narok, zilisababisha familia kadhaa kuhama makazi yao baada ya washambuliaji kuchoma moto nyumba na mali.

Kufikia jana Jumapili 30/08/2025, hali ya wasiwasi bado ilikuwa juu wakaazi walipofunga sehemu za Barabara ya Nakuru -Narok huko Mwisho Wa Lami, wakipinga mauaji hayo na kudai serikali iingilie kati.

Kufuatia ghasia hizo, serikali imepeleka maafisa wa usalama eneo hilo kurejesha utulivu.

SOMA HIZI HAPA:

HABARI PICHA: Jionee RC Balozi Batilda Buriani alivyopokea Mwenge wa Uhuru Jijini Tanga

ANGALIA NAFASI MPYA ZA KAZI HAPA:

0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.