Fuya Kimbita achukua fomu Jimbo la Hai,asema ni wakati sahihi kumsaidia mbunge aliyekuwepo kumalizia aliyoanza

Masama BlogMATUKIOKITAIFASIASA5 months ago193 Views

Kada wa Chama Cha Mapinduzi Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro Ndg.Fuya Godwin Kimbita amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi ili kupeperusha bendera ya Chama hicho katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.

Aidha Ndugu Fuya aliyefika ofisi za CCM Hai majira ya saa mbili kamili asubuhi juzi jumamosi 28/06/2025 ambapo baada ya Kuchukua Fomu hiyo katika ofisi ya CCM iliyopo Bomang’ombe Wilayani Hai amesema amefurahi na anamshukuru sana Mungu kumfikisha siku ya leo kwani yeye na wana Hai wameisubiri siku hiyo kwa Hamu kubwa.

Kimbita amesema Mbunge aliyopo Madarakani Mhe.Saashisha Mafuwe kwa nafasi yake amefanya kazi nzuri na sasa ni muda wa kuwaacha wengine wamsaidie kwani bado zipo kazi alizozianza tangu 2020 hazijakamilika ila yeye ndiye mwenye mwarobaini wa kuzikamilisha kama alivyofanya 2005 hadi 2010 akiwa mbunge kipindi cha serikali ya awamu ya 4.

Mbali na kuwa mwanachama mwaminifu wa Chama cha Mapinduzi Bw.Fuya amewahi kuwa mbunge wa Hai 2005 hadi 2010, mjumbe wa Halmshauri kuu (NEC) ya CCM,Mjumbe wa kamati mbalimbali za Bunge,Mjumbe wa kamati za kusaidia Maendeleo ya Chama Cha Mapinduzi ikiwepo kuwa Mwasisi wa haraambee ya umaliziaji wa ujenzi wa Ofisi ya CCM wilayani hai.

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...