DIAMOND PLATNUMZ AWA GUMZO TUZO ZA BET AWARDS,ANGALIA MAMBO YAKE

Admin Updates10 years ago6 Views



Staa wa Bongo Fleva ambaye kwa sasa
anafanya kweli kimataifa, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ameandika
historia kwenye Tuzo za Black Entertainment Television (BET) 2014 huku
akiwatia kiwewe mastaa wakubwa kama Cornell Iral Haynes ‘Nelly’,
Christopher Maurice ‘Chris Brown’ na wengine kibao.


Diamond akisalimiana na Nelly.



Tukio hilo lilijiri usiku wa kuamkia Jumatatu wiki hii kwenye Ukumbi
wa Nokia Theatre jijini Los Angeles, Marekani ambapo Diamond alikuwa
ameteuliwa kuwania Kipengele cha Mwanamuziki Bora kutoka Afrika akiwa
sambamba na mwanamuziki Davido (Nigeria), Mafikizolo (Afrika Kusini),
Tiwa Savage (Nigeria), Toofan (Togo) na Sarkodie (Ghana).



TUZO YAENDA KWA DAVIDO

Tuzo hiyo haikuwa bahati kwa Diamond kwani ilikwenda kwa Davido.


Licha ya kukosa tuzo hiyo, yapo mengi ambayo Diamond ameweka historia au
rekodi katika ‘event’ huku kuunganishwa na mastaa hao ikiwa topiki
muhimu.



MCHUMBA WA CHRISS BROWN AMSHOBOKEA

Katika hali ya kushangaza, mwanamitindo maarufu Marekani ambaye ni
mchumba wa Chris Brown, Karrueche Tran alionekana kumshobokea Diamond
mara alipokutana naye uso kwa uso.


Karrueche alijikuta hajiwezi alipokuwa  akimhoji Diamond ambapo moja kwa
moja alimvutia kipaza sauti na kuanza kumpiga maswali huku akionesha
kuvutiwa naye kwa muonekano aliokuwa nao.

Diamond akihojiwa na demu wa Chris Brown.



Karrueche alikuwa akijichekeshachekesha huku akimhoji kuhusiana na
mwanamuziki ambaye Diamond anamkubali ambapo alijibu ni Chris Brown,
wote wakajikuta wakiangua kicheko.


Kana kwamba hiyo haitoshi, Karrueche muda wote aliendelea kumshangaa na mwisho wa siku wakabadilishana namba za simu.

MASTAA MACHO JUU

Ulipofika wakati wa utoaji tuzo katika kategori ya Mwanamuziki Bora
kutoka Afrika, lilipotajwa tu jina la Diamond kutoka Tanzania na wimbo
wake wa Number One RMX, mastaa kibao walionesha kushangaa na ndipo macho
yote yakahamia eneo aliokuwa amekaa.


Wengi walionekana kutoa maneno ya chinichini sambamba na kumuoneshea vidole wakionesha kumkubali kwa kutinga mjengoni hapo.

NELLY, CHRIS BROWN WAINGIWA KIWEWE

Wakati Diamond anaingia ukumbini, mastaa mbalimbali duniani walionekana
kumshangaa na kati yao alikuwa ni Nelly ambaye aliushikilia mkono wa
Diamond kwa sekunde kadhaa akitaka waendelee kupiga stori.


Diamond akiwa kwenye pozi



Wakiwa katika zulia maalum jekundu, Nelly aliyewahi kutamba na wimbo
wake maarufu wa Dilemma alionekana na kutaka kumfahamu zaidi Diamond.

Kila sehemu aliyokuwa akienda, Nelly hakutaka kumuacha na alionekana
kuambatana naye kwa kumng’ang’ania mkono kila kona akipiga naye picha na
kuzunguka eneo lote wakiwa pamoja.


Naye Chris Brown ambaye aliangusha bonge la shoo alionekana kumshangaa Diamond huku akitamani kuendelea kukaa naye.

Kwa mujibu wa shuhuda wetu ukumbini humo, maswali mengi yaliibuka
kuwa iweje, kwa Mtanzania kama yule kukanyaga katika mjengo mmoja na
mstaa wa dunia.

TYSON, MAYWEATHER WADUWAA

Mabondia maarufu duniani akiwemo Floyd Mayweather na Mike Tyson
walijikuta wakiduwaa kwa kumshangaa kwa kila hatua aliyokuwa anapiga.
Macho yao hayakuwa mbali naye na hata katika zulia jekundu, Maywearher,
baada ya kumaliza kupiga picha akiwa na mkewe alimfuata Diamond na
kuongea naye mawili-matatu kuonesha kukumkubali.

MASTAA KIBAO WAGOMBEA NAMBA

Wakati shoo hiyo ikiendelea baadhi ya msataa waliokuwa pembeni na 
Diamond walionekana kumfagilia na hata wengine kuomba namba za simu kwa
malengo tofauti ikiwa ni pamoja na kutaka kufanya naye kolabo katika
siku za usoni.


Cornell Iral Haynes ‘Nelly’, akiwa kwenye pozi



LUPITA, DIAMOND USO KWA USO


Staa kutoka Kenya ambaye anatingisha katika soko la filamu za Hollywood,
Marekani kupitia filamu ya 12 Years A Slave, Lupita Nyng’o alikutana
uso kwa uso na Diamond wakiwa wote wametokea Ukanda wa Afrika ya
Mashariki.

Walionekana kuwa na furaha kwa pamoja na ikumbukwe kuwa Lupita
amejizolewa umaarufu mkubwa ambapo hata Jay-Z na Rihanna waliwahi
kuandika kupitia kurasa zao kwenye mitandao ya kijamii wakioneshwa
kumkubali kwa kazi zake.

Mastaa wengine wakubwa aliokutana nao ni pamoja na Ashanti, DJ
khalid, Jeniffer Hudson, French Montana, John Legend, Paris Hilton na
wengine kibao

HABARI NYUMA YA PAZI

Duru za kibahari zilieleza kwamba mambo yote yanayokea kwa Diamond kuna
nguvu kubwa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete
ambaye hivi karibuni alimkutanisha mtoto huyo wa Tandale na meneja wa
wanamuziki wakubwa duniani, Tremaine Neverson ‘Trey Songz’ na Sean
Michael Leonard Anderson ‘Big Sean’, ili kufanya nao kazi.

“Siyo jambo rahisi na bado milango itazidi kufunguka zaidi kwani JK
aliahidi kumsaidia. Kwa kuunganishwa na mastaa wakubwa duniani sasa hivi
utasikia amehamia Marekani kutusua mtonyo,” alisema mmoja wa wasanii wa
Bongo Fleva ambaye naye anafanya vizuri.


Christopher Maurice ‘Chris Brown’ akiwa kwenye pozi



Akizungumza na mwanahabari wetu kutoka jijini Los Angeles, Diamond
alisema kuwa hakuamini jinsi alivyopokelewa na mastaa wakubwa ambao
hakutarajia kukutana nao uso kwa uso.


“Sasa najua ndoto itatimia. Mastaa wakubwa lakini wamenionesha upendo wa
ajabu. Naona wasanii wote duniani wanapendana sana. Jamaa hawana
ubaguzi. Walinichangamkia sana utadhani tunafahamiana.

“Kuna mengi nafanya nao lakini siwezi kuwataja kwa sababu si unawajua Wabongo?

“Lakini nikidondoka tu Bongo naachia video mbili kali sana, mashabiki wangu wasikilizie.


“Kuhusu kukosa tuzo, mimi naona ni mwanzo mzuri. Inanipa hasira ya
kutengeneza muziki mzuri utakaopendwa na watu wengi duniani. Tusikate
tamaa, ni mwanzo mzuri. Pia asiyekubali kushindwa si mshindani,”
alifunguka Diamond akimshukuru Mungu kwa yote anayomtendea kila kukicha
kisha watu wanampa sapoti.


Mike Tyson akiwa kwenye pozi



SASA LEVO ZA AKINA HASHEEM THABEET


Kwa sasa Diamond anakuwa ni staa mwingine wa Kibongo wa kimataifa
akitanguliwa na staa wa NBA, Hasheem Thabeet, Modo Flaviana Matata na
wengineo.

0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...