CCM Yafunika Uzinduzi Kampeni Kawe,Dr Samia Atangaza Neema

Masama BlogMATUKIO5 months ago275 Views

CCM Yafunika Uzinduzi Kampeni Kawe

Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan, amewataka wagombea wote wa nafasi za udiwani na ubunge kupitia chama hicho kuwafikia wananchi katika kipindi hiki cha kampeni na kuwaeleza kuhusu utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/25, pamoja na mipango na sera za chama kuelekea mwaka 2030.

Aidha, katika hotuba yake, Rais Samia mbali na kueleza mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake pamoja na vipaumbele vya sasa, aliwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi katika mikutano ya kampeni ya wagombea wa CCM ili kupata fursa ya kusikiliza sera na mipango ya chama.

Alisisitiza kuwa kufanya hivyo kutawaweka wananchi katika nafasi nzuri ya kufanya maamuzi sahihi ya kuwachagua viongozi bora watakaowaletea maendeleo katika miaka mitano ijayo.

Akizungumza, Agosti 28, 2025, mbele ya umati wa wananchi waliojitokeza katika viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe, Kinondoni, jijini Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za kitaifa za CCM, Rais Samia – akiambatana na mgombea mwenza wake, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi – aliwashukuru wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam pamoja na mikoa jirani kwa kujitokeza kwa wingi.

Alisema nguvu ya CCM imejengwa katika misingi ya umoja, amani na mshikamano miongoni mwa Watanzania.

SOMA HIZI:

RC Senyamule aelekeza Vikundi zaidi ya 300 Jijini Dodoma Vipewe mikopo Tsh Bilioni 3.6

0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.