BASATA WAMPA BARAKA ZOTE MISS UNIVERSE KWENDA KUWAKILISHA NCHI

6 years ago92 Views

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limemkabidhi bendera mwakilishi wa mashindano ya Ulimbwende ya dunia ya  Miss Universe 2019 yanayotarajia kufanyika Jiji la Atlanta nchini Marekani.

Mashindano hayo yatafanyika Desemba 08 mwaka huu, na kwa Tanzania yatawakilishwa na Shubila Stanton Kaigarula (23) Miss Universe Tanzania ambaye anasafiri leo Novemba 27 kwenda kuliwakilisha Taifa kwenye mashindano ya ulimbwende ya Miss Universe nchini Marekani. 

Katibu Mtendaji  Godfrey Mngereza amekabidhi bendera kwa mrembo huyo na ameitumia nafasi hii kuwaasa Wasanii wengine nchini wajijengee tabia ya kuaga ili kupata baraka za Serikali.

 Amesema, pindi wanapohitajika kusafiri kwenda kuliwakilisha Taifa kwenye mashindano mbalimbali ni muhimu serikali kufahamu na hilo linajenga taswira nzuri kwa taifa.
 Katibu Mtendaji wa BASATA Godfrey Mngereza akikabidhi bendera kwa Mwakilishi wa Tanzania kwenye mashindano ya ulimbwende Miss Universe 2019 yanayotarajia kufanyika Jiji la Atlanta Nchini Marekani Desemba 12 mwaka huu

from MICHUZI BLOG https://ift.tt/35NWrU7
via

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.