HUSSEIN BASHE AWACHANA UKAWA..AWAPA KAULI NZITOO..MSIKIE HAPA

Admin Updates9 years ago5 Views

MGOMBEA ubunge wa CCM katika Jimbo la Nzega Mjini, Hussein Bashe, amesema wapinzani wanataka kuwagawa wananchi kwa misingi ya udini na ukabila.

Akihutubia katika mkutano wa kampeni katika mji wa Ndala wilayani Nzega alisema kwa miaka mingi watanzania wameishi kwa umoja bila kujali ukabila na udini, lakini wapinzani wanataka kuleta mambo hayo kwa lengo la kuwagawa Watanzania. “Hawa wanakuja kutugawa kwa ukabila na udini, msikubali kugawanywa kwa misingi ya udini na ukabila, ichagueni CCM tuendelee kubaki wamoja,” alisema Bashe. Mgombea huyo ambaye anafahamika kuwa mtu wa karibu na mgombea urais wa Lowassa kutokana na kuwa msemaji wa Kambi ya Lowassa wakati wa mchakato wa kusaka urais kwa tiketi ya CCM, alisema mabadiliko yanayohubiriwa na wapinzani yameshafanywa na CCM. “Vijana wenzangu nawaombeni kama ni mabadiliko tuyatafute ndani ya CCM, wanasema eti CCM ni ile ile haifanyi kitu, mimi nawaambia CCM ni ile ile ila madereva tofauti. “Safari hii dereva ni Magufuli, kondakta ni Mama Samia na sisi akina Bashe, Kigwangala (Hamisi) ni mautingo na safari itakuwa salama,” alisema Bashe.
Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.