MGOMBEA ubunge wa CCM katika Jimbo la Nzega Mjini, Hussein Bashe, amesema wapinzani wanataka kuwagawa wananchi kwa misingi ya udini na ukabila.
Akihutubia katika mkutano wa kampeni katika mji wa Ndala wilayani Nzega alisema kwa miaka mingi watanzania wameishi kwa umoja bila kujali ukabila na udini, lakini wapinzani wanataka kuleta mambo hayo kwa lengo la kuwagawa Watanzania. “Hawa wanakuja kutugawa kwa ukabila na udini, msikubali kugawanywa kwa misingi ya udini na ukabila, ichagueni CCM tuendelee kubaki wamoja,” alisema Bashe. Mgombea huyo ambaye anafahamika kuwa mtu wa karibu na mgombea urais wa Lowassa kutokana na kuwa msemaji wa Kambi ya Lowassa wakati wa mchakato wa kusaka urais kwa tiketi ya CCM, alisema mabadiliko yanayohubiriwa na wapinzani yameshafanywa na CCM. “Vijana wenzangu nawaombeni kama ni mabadiliko tuyatafute ndani ya CCM, wanasema eti CCM ni ile ile haifanyi kitu, mimi nawaambia CCM ni ile ile ila madereva tofauti. “Safari hii dereva ni Magufuli, kondakta ni Mama Samia na sisi akina Bashe, Kigwangala (Hamisi) ni mautingo na safari itakuwa salama,” alisema Bashe.
Recommended Products
-
2025 Summer Rapper Feid Ferxxo Men’s Cotton Fashion Hip-hop T-shirt Casual and Comfortable Short-sleeved T-shirt Street Wear
Affliate products $22.00 -
3 IN 1 Magnetic Folding Wireless Charger Station For IPhone Transparent Fast Charging For IWatch And Airpods
Affliate products -
Grandpa Of Love hoodies Human French Letters Dad Papa Papy Gift Men Clothing hoodies
Affliate products $22.00 -
Sale!
Lenovo D18 Drone 8K Aerial HD Dual-Camera Intelligent Obstacle Avoidance Brushless Power 5G WIFI Screen Remote Control GPS Drone
Affliate products Original price was: $7.99.$7.89Current price is: $7.89. -
Mini Portable Face Cordless Shavers Rechargeable USB Electric Shaver Wet & Dry Painless Small Size Machine Shaving For Men
Affliate products $44.00 -
New Original T75 Bone Conduction Wireless Bluetooth 5.3 Headphones Sports Earphones HiFi Sound Quality Waterproof TWS Headset
Affliate products $3.33





