Wanaosema Nimeachana na Iyobo Watasubiri Sana- Aunty Ezekiel

Special Correspondent6 years ago8 Views

Msanii wa filamu za Bongo movie Aunty Ezekiel amefunguka kuhusu mahusiano yake na Mpenzi Wake ambaye ni dancer wa WCB Moses Iyobo.

Aunty Ezekiel amefunguka na kuweka wazi kuwa amekuwa akishangazwa na tetesi zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii hivi sasa kuwa yeye ameachana na Baba watoto wake Mose Iyobo.



Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Aunt alisema afikiri katika dunia hii hata kama unapenda na mtu kwa kiasi gani hamuwezi kuishi bila kutokea ugomvi wowote kwa sababu wao sio malaika lakini wanapogombana wanayamaliza na maisha yanaendelea kama kawaida lakini inavyoonekana kuna watu wanataka kuona penzi lao likisambaratika kabisa.



Nafikiri wanaosema tumeachana watasubiri sana kama kugombana hakuna wanaoishi kama malaika, kwa sababu wote ni binadamu lakini hatuna ugomvi endelevu, yule ni mzazi mwenzangu na wanaosubiri tuachane tutawaacha mbali sana”.

Tetesi za Aunty Ezekiel na Mose kuachana Zilianza mara Baada ya wawili hao kutoonekana kwenye mitandao ya kijamii pamoja na zilipamba moto zaidi Baada ya Aunty kumuacha Mose Tanzania alipoenda kusheherekea birthday yake Dubai.


Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.