WAISLAMU WAOMBA KUJITOKEZA KUSHIRIKI RAMADHANI MARATHON

7 years ago103 Views

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Tasisi ya Pink Hijab Initiatives imeandaa mbio na Matembezi ya Kilometa kumi kuanzia Viwanja vya Green Ground Osterbay na kuishia katika Viwanja hivyo kwa kupitia barabara ya  Kenyata, Chole Road,Karume Road , Haile Salasi Road kupitia Coco Beach na kurudi katika Viwanjani hapo.

akizungumza na Globu ya Jamii Mratibu wa Mbio hizo kutoka Pink Hijab Initiative, Alhaj Jamal Mwarab Khalfan amesema kuwa lengo la mbio hizo ni kusaidia watoto waliopo katika Mazingira hatarishi katika Mkoa wa Tanga Wilaya ya Pangani.

“Sisi kama Tasisi ya Kislamu tumeona vyema kuitumia Ramdhani hii kama sehemu ya kurudisha tunachokipata kwa jamii kwa kuandaa mbio hizi na matembezi hili tuweze kuwasaidia watoto wetu waliopo katika Wilaya ya Pangani hivyo tunawaomba wote wenye mapenzi mema na watoto wetu kuja kujumuika na sisi April 21 Mwaka huu”amesema Alhaj Jamal.

Amesema mtu anayependa kushiriki mbio hizi anaweza kuchangia kiasi cha shilingi 20,000/-pia naweza kuwasiliana nasi kupitia namba 0713433407 au 0655445105 hili aweze kushiriki na kuchangia zaidi.

from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2IbEFCp
via

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.