
Mafie aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake Temeke Dar es Salaam ambapo alisema imekuwepo na changamoto hiyo ya watu kushindwa kudai risti pindi wanapofanya manunuzi.
Amefafua kuwa Mara nyingi wafanyabiashara na hata wateja hawana tabia ya kudai risti na kutoa hivyo basi TRA inawakumbusha kutekeleza sheria na kushindwa kufanya hivyo nikosa kama alivyotangulia kusema .
Amesema pindi mteja anapopewa risti au kutoa risti hiyo imeunganishwa kwenye mfumo wa ndani wa TRA ambayo inawezssha kujua kwamba ameuza au hajauza.
Akizungumzia Utoaji wa elimu alisema wao kama TRA wanajitahidi kutoa elimu kwa wafanyabiashara na hivi sasa wanajipanga kutoa elimu kwa kina kutokana na mabadiliko ambayo yamefanyika kupitia Bunge.
Amesema kwa asilimia 77 wanatoa elimu na wanaendelea kutoa elimu hiyo na kusisitiza kuwa ulipaji wa kodi ni lazima kwa kila mtanzania kulipa kodi ili mambo mengine katika nchi yaende.
Meneja Mafie alisema wanakuwa na mahusiano mazuri na walipa kodi japo wakati mwingine kunakuwa na hali ya kukimbizana nakwamba hiyo inatokana na baadhi ya wafanyabiashara kukwepa kulipa kodi.
” katika jambo hili ndugu waandishi hapa nishauri Serikali kuona namna ya kuazisha elimu kupitia elimu ya msingi ili.mwanafunzi anapoendelea kupata elimu basi ajuwe ipasavyo kuhusu kodi.” Alisema Meneja
Mmoja wa maofisa wanaotoa elimu ya huduma kwa mlipa kodi Paul Magembe alisema wanafanya kazi hiyo kwa kuwatembelea vikundi mbalimbali ili kuwapa elimu ili kuona umuhimu wa kulipa kodi katika jambo ambalo wanalifanya.
from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2Ip1B0Q
via






