BARAZA LA KILIMO LAWAKUTANISHA WADAU WA KILIMO KUIJADILI ASDP II.

6 years ago72 Views


Mjumbe wa Bodi ya wakurugenzi ya baraza la kilimo Tanzania Bw Enock Ndondole akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau wa sekta binafsi katika kilimo, kwa niaba ya mwenyekiti wa Bodi, Mkutano huo umefanyika mkoani morogoro na kuhudhuliwa na wadau mbalimbali katika sekta ya kilimo.
Mkurugenzi wa Sera Baraza la Kilimo Tanzania Bw. Timothy Mmbaga akifafanua jambo wakati wa mkutano huo uliokuwa ukijadili mchango wao sekta binafsi katika utekelezaji wa mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo nchini ASDP II.
Sehemu ya washiriki wa mkutano huo wa siku moja ulioandaliwa na Baraza la kilimo Tanzania na kufanyika Mkoani Morogoro.
Mkurugenzi Msaidizi wa sera na Mipango Wizara ya Kilimo Bw. Osward Ruboha,(wa kwanza) Makamo mwenyekiti Baraza la Kilimo Mh Jitu Son na Mjumbe wa Bodi wa Baraza la Kilimo wakifuatilia kwa makini mjadala uliokuwa ukiendelea katika Mkutano huo wa Sekta binafsi katika Kilimo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Sera na Mipango Wizara ya Kilimo Bw. Osward Ruboha kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo.(Mwenye suti nyeusi kwa walioketi) akiwa katika Picha ya pamoja na wajumbe wa Mkutano wa Sekta binafsi katika Kilimo.

Baraza la kilimo Tanzania limewakutanisha wadau wa sekta binafsi katika kilimo ili kujadili mchango wao katika utekelezaji wa mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo nchini ASDP II.

Mkutano huo wa siku moja umefanyika Mkoani Morogoro na kuhudhuliwa na wadau zaidi ya 60 wakiwemo maafisa wa Serikali, Taasisi za Kilimo na wadau wa Kilimo ambapo ulifunguliwa na Mkurugenzi Msaidizi wa sera na Mipango Wizara ya Kilimo Bw. Osward Ruboha kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo.

from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2WAZ0rC
via

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.