Mwili wa Etienne Tshisekedi wapata maziko ya kitaifa DR Congo

6 years ago71 Views

 Kwa wafuasi wake sherehe hiyo ya misa ya wafu ni ushindi dhidi ya serikali iliokuwepo
 
Jeneza la marehemu Etienne Tshisekedi likibebwa

 Rais wa Rwanda Paul kagame akitoa heshima zake za mwisho
 Wale waliopata wito rasmi waliruhusiwa kuingia

 Kulikuwa na biashara ya mau nje ya uwanja huo
Wafuasi wa mkongwe huyo wa upinzani walihudhuria mazishi yake


Miaka miwili baada ya kifo chake nchini Ubelgiji, mazishi ya kitaifa yamefanyika kwa kiongozi wa zamani wa upinzani nchini DR Congo Etienne Tshisekedi.

Mwili wake ulisafirishwa nyumbani siku ya Alhamisi kufuatia mgogoro kati ya familia yake na serikali ya iliopita .
Mgogoro huo ulikwisha baada ya mwanawe kuwa rais mwaka uliopita.
Makumi ya maelfu ya watu walihudhuria Ibada ya wafu katika uwanja wa mashahidi mjini Kinshasa wakiongozwa na Askofu Fridolin Ambongo.
Kanisa katoliki lenye ushawishi mkubwa nchini humo liliwataka wafuasi wake kuhudhuri kwa wingi katika mazishi hayo.
Siku ya Ijumaa , rais wa Rwanda na Angola walikua miongoni mwa idadi kubwa ya watu waliojitokeza ili kutoa heshima yao ya mwisho kwa marehemu kufuatia miaka kadhaa ya uhasama kati ya taifa lake na DR Congo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA BBC Swahili.

from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2MjZ3DZ
via

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.