JOSEPH MPNAGALA-MTWARA
Serikali imesema itaendelea kuimarisha Mafunzo kwa walim wa michezo ili kuweza kuwa na Walim watakaoweza kuibua Vipaji vya wanafunzi Mashuleni na kuweza kusaidia Taifa katika michezo mbalimbali.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi na Prf.Joyce Ndalichako wakati akifunga mafunzo ya Copa cocacola UMISETA yaliyomaliziaka katika Uwanja wa Umoja Nangwanda Sijaona Mkoani Mtwara.
Prf.Ndalichako amesema michezo ya umiseta imekuwa ikiibua vipaji mbalimbali kutoka kwa vijana na wapo waliofanikiwa katika ngazi ya kitaifa na kimataifa hivyo serikali itaendelea kuimarisha michezo.
“Tunafaham Kwamba michezo inasaidia kuimarisha afya michezo inasaidia kupunguza na kuepusha kupata magonjwa yasiyoambukiza lakini kwa wanafunzi Michezo inasaidia kuchangamsha akili”amesema PRf Ndalichako.
Naye Meneja Maendeleo ya Biashara Kampuni ya Coca Cola Yassin Hussein amesema ili kuhakikisha Mazingira yanatunzwa kampuni yake imeanzisha kampeni ya Rejesha na Ushinde ambapo Wanafunzi wanashindana kukusanya Chupa za zilizotumika.
“Kampeni yetu ya cocacoLA vijana wameweza kukusanya Chupa za Plastic zilizotumika zoezi ambalo tumelianzisha mwezi June na litamalizika mwezi wa Nane ili kuhakikisha tunatunza mazingira na nchi yetu inabaki salama”amesema Yassin.
Michezo ya Umeseta imeshirikisha Mikoa26 ambapo Fainali zilikutanisha Timu ya Songwe na Ruvuma ambapo Timu ya Ruvuma Ilishinda kwa mikwaju ya penati 10 kwa 9 .

Baadhi ya wanfunzi wa kutoka shule mbalimbali za sekondari wakionesha ishara ya kumalizika kwa mashindano ya Copa Coca Cola ambayo yalimalizika katika Uwanja wa Umoja Nangwanda Sijaona Mkoani Mtwara

Wachezaji na mashabiki wa timu ya Mkoa wa Ruvuma wakimnyanyua Juu Kipa wa Timu hiyo baada ya Kufanikiwa kupangua Mkwaju wa Mwisho uliyoipa Timu ya Mkoa wa Ruvuma Ushindi.
from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2IzUUIr
via
