Watu wenye Ulemavu waiomba Tume ya Uchaguzi kuwawekea Mazingira Rafiki

6 years ago60 Views

Mbarouk Salim ni Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Taifa akizungumza na na Watu wenye ulemavu (hawapopichani)

Na.Vero Ignatus,Arusha.
Watu wenye Ulemavu mkoa wa Arusha wameiomba Tume ya uchaguzi kuweka mazingira rafiki kwao ili waweze kushiriki katika zoezi la uandikishaji wa daftrari la wapiga kura na kutimiza haki yao ya kikatiba bila kupata vikwazo vinavyotokana na hali zao.

Yunisi Urassa ni Katibu wa Shirikisho la vyama vya Walemavu wilaya ya Arusha ametoa maombi hayo huku akisisitiza kuwepo kwa mazingira rafiki katika vituo vya kujiandikisha ili viweze kufikika kwa urahisi na watu wote katika kikao cha Tume ya Uchaguzi na wadau wa Uchaguzi wakiwemo wawakilishi wa vyama vya siasa,wawakilishi wa makundi maalumu katika jamii.
Mbarouk Salim ni Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Taifa amesema kuwa zoezi hilo litaanza hivi karibuni na tayari ziko asasi za kiraia zilizopewa kibali cha kutoa elimu za raia kwa wapiga kura ili waweze kutumia haki yao ya kikatiba.
Wajumbe kutoka katika vyama vya siasa Denis Mwita Katibu wa Ccm wilaya ya Arusha na Innocent Joseph ambaye ni Katibu wa Chadema Wilaya ya Arusha wameiomba tume hiyo kuweka vituo karibu na makazi ya wananchi pamoja na kuhakikisha kuwa sheria za Uchaguzi zinazingatiwa.

from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2S2jCUI
via

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.