Benki ya Stanbic yatoa msaada wa vifaa tiba kwa hospitali ya taifa ya Muhimbili.

6 years ago71 Views

Mkuu wa kitengo cha Mikopo wa benki ya Stanbic Bank, Bwana Daniel Mbotto akimkabidhi baadhi ya vifaa tiba kwa mkuu wa jengo la wazazi block 2 katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Bi. Suzan Ndambala hivi karibuni kama sehemu ya kuchangia upatikanaji wa huduma bora kwa kwa watoto wanaozaliwa na matatizo katika mfumo wa kupumua. Benki ya Stanbic imetoa mchango huo kama sehemu ya juhudi zake za kuchangia jamii katika sekta ya afya na elimu. Wengine katika picha ni wafanyakazi wa benki na MNH. 
Mkuu wa kitengo Cha Mazingira ya Ndani kutoka hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Bi. Ester Mwambogoja (katikati) akiwashukuru baadhi ya wafanyakazi kutoka Benki ya Stanbic baada ya kupokea msaada wa vifaa tiba vilivyotolewa na benki hiyo hivi karibuni. Madhumuni ya kutoa vifaa hivyo ni kuchangia upatikanaji wa huduma bora kwa watoto wanaozaliwa na matatizo katika mfumo wa kupumua. Hii ni sehemu ya juhudi za Benki ya Stanbic katika kuchangia sekta ya afya na elimu katika jamii. Wengine katika picha ni wafanyakazi wa MNH.

from MICHUZI BLOG https://ift.tt/32lpVrw
via

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.