Hivi ndivyo Imamu wa Mapenzi ya Jinsia Moja Alivyouawa

Admin Updates3 months ago25 Views

 Imamu wa Mapenzi ya Jinsia Moja Auawa

Imamu wa kwanza duniani aliyejitangaza hadharani kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja, Muhsin Hendricks (57), ameuawa kwa kupigwa risasi nchini Afrika Kusini huku ripoti zikisema ameuawa baada ya kufungisha ndoa ya Watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.

Imamu huyo alikuwa anaongoza Msikiti mmoja JijiniCape Town uliolenga kuwa mahali salama na kimbilio kwa Waumini wa kiislamu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja na wale waliotengwa na jamii ambapo alipigwa risasi Jumamosi asubuhi baada ya gari alilokuwa akisafiria karibu na jiji la kusini la Gqeberha kushambuliwa.

Polisi wamesema “Washukiwa wawili wasiojulikana wakiwa wamefunika nyuso zao walitoka kwenye gari nyingine na kuanza kulimiminia risasi nyingi gari hilo”

Habari za kifo cha Hendricks zimeleta mshtuko mkubwa katika jamii ya Watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja (LGBTQ+ ) na kwingineko, huku kukitolewa salamu nyingi za rambirambi kutoka sehemu mbalimbali za dunia.

Taarifa za tukio hilo zimeonekana kupitia video za CCTV zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii ambapo video hiyo inaonesha gari likisimama na kuziba njia ya gari alilokuwamo Hendricks kabla ya kuanza kushambuliwa.

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.