
WAZIRI Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye aliyekuwa amelazwa katika Taasisi ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete iliyoko Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), ameruhusiwa kurudi nyumbani.
Ofisa Uhusiano Msaidizi wa MNH, John Steven, jana alisema Sumaye aliruhusiwa juzi jioni baada ya madaktari kuridhishwa na maendeleo ya afya yake.
“Sumaye amepewa ruhusa ya kurudi nyumbani tangu juzi jioni, madaktari wake waliridhishwa na mwenendo wa afya yake kutokana na matibabu waliyompatia dhidi ya ugonjwa uliokuwa unamsumbua,”alisema.
Hata hivyo, Steven hakufafanua ugonjwa uliokuwa ukimsumbua kiongozi huyo mstaafu kwa kile alichoeleza kuwa kanuni na sheria za kitabibu zinakataza.
“Siwezi kutaja ugonjwa uliomfanya akalazwa hapa, mwenyewe anaweza kuwaeleza kwa sababu ni siri yake na daktari wake,” alisema.
Sumaye alilazwa hospitalini hapo Januari 7, mwaka huu na Januari 11, Rais John Magufuli, alimtembelea hospitalini hapo na kumpa pole.
Mapema mwaka huu, Sumaye alitangaza rasmi kujiunga na Chadema baada ya kuondoka katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwaka jana muda mfupi kabla ya kampeni za uchaguzi.
Recommended Products
-
2025 Summer Rapper Feid Ferxxo Men’s Cotton Fashion Hip-hop T-shirt Casual and Comfortable Short-sleeved T-shirt Street Wear
Affliate products $22.00 -
3 IN 1 Magnetic Folding Wireless Charger Station For IPhone Transparent Fast Charging For IWatch And Airpods
Affliate products -
Grandpa Of Love hoodies Human French Letters Dad Papa Papy Gift Men Clothing hoodies
Affliate products $22.00 -
Sale!
Lenovo D18 Drone 8K Aerial HD Dual-Camera Intelligent Obstacle Avoidance Brushless Power 5G WIFI Screen Remote Control GPS Drone
Affliate products Original price was: $7.99.$7.89Current price is: $7.89. -
Mini Portable Face Cordless Shavers Rechargeable USB Electric Shaver Wet & Dry Painless Small Size Machine Shaving For Men
Affliate products $44.00 -
New Original T75 Bone Conduction Wireless Bluetooth 5.3 Headphones Sports Earphones HiFi Sound Quality Waterproof TWS Headset
Affliate products $3.33






