Ruto aahidi Tsh Milioni 48 kwa Kila Mchezaji Harambee Stars!

Masama BlogKIMATAIFAMICHEZO5 months ago164 Views

Rais wa Kenya, William Ruto, leo amekutana na kikosi cha Harambee Stars na kutoa ahadi nono kuelekea mechi ya mwisho ya Kundi A ya michuano ya CHAN 2024 dhidi ya Zambia, itakayopigwa Jumapili katika Uwanja wa Kasarani.

Ruto amethibitisha kutimiza ahadi yake ya awali ya kuwapa wachezaji KSh milioni 1 (TSH 19.2 milioni) kila mmoja kwa kila ushindi wa mechi za makundi, lakini safari hii ameongeza dau, akiahidi KSh milioni 2.5 (TSh 48 milioni) kwa kila mchezaji endapo wataibuka na ushindi dhidi ya Zambia.

Zaidi ya hapo, Rais Ruto ameahidi kutoa KSh milioni 1 (TSH 19.2 milioni) na nyumba ya bei nafuu kwa kila mchezaji iwapo Harambee Stars watashinda mchezo wa robo fainali ya CHAN 2024.

Ahadi hizo zimechochea ari ya wachezaji na mashabiki, huku matumaini yakiwa juu kwamba timu hiyo itaandika historia mpya kwenye mashindano hayo.

SOMA HABARI ZA MICHEZO ZAIDI HAPA

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.