
ESTERLINA Sanga ukipenda waweza kumuita Linah au Ndege Mnana, ni mmoja wa mastaa wa Muziki wa Bongo Fleva aliyepotea kwa muda kutokana na pilika za uzazi. Linah anayebamba na nyimbo zake nyingi zikiwemo No Stress, Kosa Sina, Raha Jipe Mwenyewe na Malkia wa Nguvu kwa sasa ni mama wa mtoto mmoja aliyempa jina la Tracy Paris ambaye amezaa na mchumba anayefahamika kwa jina moja la Shaban.
Ijumaa limemfungia kazi na kufanya naye mahojiano moja kwa moja akiwa kwenye studio yake pande za Tegeta jijini Dar na katika makala haya amefunguka mengi likiwemo la kutaka kuolewa na mchumba wake huyo ambaye wapo tofauti kiimani.
Ijumaa: Wanamuziki wengi wamekuwa wakijishauri sana katika suala zima la kubeba ujauzito kutokana na kazi zao, wewe halikukuumiza kichwa hili?
Linah: Kwa sababu niliamua kwa moyo mmoja kabisa wala hilo sikujiuliza hata mara moja kwa kuwa nilitamani mtoto.
Ijumaa: Wakati unaelekea chumba cha kujifungua, muda mfupi kabla ya kuingia uliposti picha ukiwa kwenye uchungu, haikukuletea matatizo hasa kutokana na mila zetu?
Akiwa katika pozi
Linah: Kwanza ile picha sijaiposti nafikiri kulikuwa na mtu pale hospitali na pia haikuwa siku ambayo najifungua ilikuwa ni siku ambayo nilienda kuonana na daktari, sikuwa najisikia vizuri.
Ijumaa: Baba watoto wako yeye sio staa?
Linah: Hapana wala hayuko huko kabisa.
Ijumaa: Sasa mnawezaje kuendana maana mastaa kuna mambo mengi?
Linah: Unajua huyu mchumba wangu alinipenda tangu 2009, ndio kwanza naanza kutoka lakini hakupata muda wa kunifikia hivyo anajua kazi yangu na ndio maana niko nae amekubali kila kitu changu.
Ijumaa: Vipi kuhusu ndoa wewe na mchumba wako kuna matarajio hayo?
Linah: Ndiyo ni hivi karibuni.
Wakiwa na mume wake Shaban
Ijumaa: Lakini mpenzi wako ni Muislam na ninajua wazi kuwa wewe umetoka kwenye familia ya Kikristo inakuaje hili?
Linah: Ni kweli ni Muislam lakini sioni shida kuolewa naye.
Ijumaa: Kipindi cha ujauzito uliweka picha za kuonesha tumbo wazi, hiyo haikuleta shida kwa wakwe zako?
Linah: Namshukuru sana Mungu, nimepata wakwe waelewa sana kikubwa wao wanataka heshima wala hilo la picha hawalitazami.
Ijumaa: Wewe na msanii Amini mlikuwa wapenzi mnaopendana sana, vipi mkikutana sasa hivi?
Linah: Mimi na Amini tunaheshimiana sana kwa kuwa tayari ana mke wake na mimi nina mtu wangu.
Ijumaa: Asante kwa ushirikiano wako
Recommended Products
-
2025 Summer Rapper Feid Ferxxo Men’s Cotton Fashion Hip-hop T-shirt Casual and Comfortable Short-sleeved T-shirt Street Wear
Affliate products $22.00 -
3 IN 1 Magnetic Folding Wireless Charger Station For IPhone Transparent Fast Charging For IWatch And Airpods
Affliate products -
Grandpa Of Love hoodies Human French Letters Dad Papa Papy Gift Men Clothing hoodies
Affliate products $22.00 -
Sale!
Lenovo D18 Drone 8K Aerial HD Dual-Camera Intelligent Obstacle Avoidance Brushless Power 5G WIFI Screen Remote Control GPS Drone
Affliate products Original price was: $7.99.$7.89Current price is: $7.89. -
Mini Portable Face Cordless Shavers Rechargeable USB Electric Shaver Wet & Dry Painless Small Size Machine Shaving For Men
Affliate products $44.00 -
New Original T75 Bone Conduction Wireless Bluetooth 5.3 Headphones Sports Earphones HiFi Sound Quality Waterproof TWS Headset
Affliate products $3.33






