Baadhi ya wapenzi wa Muziki na Mashabiki wa Zuchu , waliohudhuria Usiku ‘Special’ kwa ajili yake ,wakifurahia Performance zinazoendelea Juu ya Stage katika onesho la Zuchu lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
Tamasha la ‘IAM ZUCHU” ni moja la Tamasha la burudani tunaweza kusema limeweza kuweka historia katika kiwanda cha burudani hapa nchini,limekuwa la aina yake kwa wale walioweza kupata fursa kuhudhulia na kushuhudia tamasha hilo.
Viongozi wa Serikali pia waliweza kufika katika tamasha hilo lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam wakiwemo Katibu Mkuu wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Hassan Abbas, Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
Wasanii wakubwa pamoja na mastaa wakubwa hapa nchini pamoja pia waliweza kufika katika tamasha hilo wakiwemo, Juma Jux, Dullvanny, Wema Sepetu,Shilole,LadyJaydee,Dulla Makabila, Flaviana Matata na wengine wengi.
Akizungumza katika Tamasha hilo Zuchu amewashukuru wapenzi wa burudani hapa nchi pamoja na wale waliowezesha tamasha hilo kufanyika hivyo ameahidi kufanya makubwa kwenye tasnia ya muziki na kuweza kufika mbali kwenye tasnia hiyo.
“Nawashukuru Watanzania Kwa Upendo wenu Mkubwa , kwa mapokezi ya Kimalkia na kunifanya niwe msanii ninaetazamwa zaidi kwasasa Afrika Mashariki”. Amesema Zuchu.
Nae Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni na Michezo Dkt. Hassan Abbasi akitoa neno kwa niaba ya Serikali amesema Serikali inathamini sana Sanaa ndio maana imemuagiza awe katika tamasha hilo, Lakini pia yeye binafsi ni Shabiki mkubwa wa @wcb_wasafi.