Arosto ya Unga Humfanya Teja Awe Mwendawazimu, Yupo Tayari Kufanya Lolote – Fanani

9 years ago104 Views

Rapper wa zamani wa kundi la HBC, Terry Fanani ambaye ni mmoja wa mastaa waliowahi kuathirika na matumizi ya dawa za kulevya, amesema arosto anayopata mteja ni kitu chenye nguvu kinachompa uchizi teja.

Akiongea na Planet Bongo ya EA Radio, Fanani amesema teja akiwa katika hali hiyo, yuko tayari kwa lolote.

“Arosto inapokukamata unakuwa katika hali ya kama mwendawazimu,” amesema.

“Kwahiyo uko tayari kufanya lolote, uko tayari kumdanganya mtu ambaye anakusaidia ili ukapate pesa ukafanye, uko tayari kuchukua hata mama yako anaumwa umepewa hela ukanunua dawa hospitali la kwanza ni kujitubu wewe kwasababu tunakuwa na ubinafsi,” amesisitiza.

“Na inapofika wakati imefika jioni sijavuta halafu sina kitu niko na kampani za washkaji tunaweza tukaingia front sio, kaba mtu chukua hela ilimradi nitibu lile tatizo langu la msingi.”

Fanani amedai yupo kwenye kipindi ambacho ameacha kutumia madawa na anapambana ili asirudie tena kwasababu kuacha si jambo rahisi.

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.