Breaking Newz: Afisa wa Polisi Akamatwa na Misokoto 40 ya Bangi..Jionee hapa

Admin Updates1 year ago5 Views

Afisa mmoja wa Polisi nchini Kenya, Kobstabo Evans Otieno amesweka rumande katika Kaunti ya Makueni akidaiwa kushiriki maandamano, huku akiwa na misokoto 40 ya bangi yenye thamani ya Shilingi 2,000.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka huduma ya Polisi -NPS, Kobstabo Otieno alikamatwa eneo la Emali katika barabara kuu ya Nairobi kuelekea Mombasa na tayari amesimamishwa kazi akisubiri kusomewa shitaka linalomkabili.

“Tunathibitisha kukamatwa kwa afisa huyo kupitia tukio lililonakiliwa kwa nambari OB:15/20/7/2023 saa nne na dakika 20 mchana na alikamatwa alipokuwa akipanga waandamanaji katika kizuizi haramu cha barabarani,” taarifa ya Mkuu wa Polisi, Japhet Koome ilisema.

Aidha, ripoti hiyo imeeleza kuwa, “Afisa huyo alikuwa miongoni mwa raia waliokuwa wakihangaisha wenye magari kwa kuwavurumishia mawe. Aidha, imebainika kuwa afisa huyo alionekana na wenzake katika mji wa Emali akiwa miongoni mwa waandamanaji waliorusha mawe katika kituo cha polisi cha Emali.”

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.