Unapokataliwa na watu kadhaa, usilichukulie swala hilo kuwa ni swala
zito saaana, kwani watu wengine wanaweza kuwa wanaamua tu, kukukatalia
kwa sababu za kijuu juu tu, zisizo na maana yoyote. Kwa mfano uoga, aibu
n.k.Unapaswa kutulia na kutojutia kwa tendo hilo, bali changamoto kama
hizi hukupatia uzoefu uzoefu katika mahusiano yenye afya.
Weka
mambo katika mtazamo, usiweke asilimia kubwa ya muda wako katika
kutengeneza mahusiano, bali jikite katika shughuli zinazokufanya upate
furaha. Kama vile kufanya kazi zako, kuwa mwenye afya, kuwa na mahusiano
mazuri na familia yako pamoja na marafiki. Utakapojikita katika kulinda
furaha yako, maisha yako yatakuwa sawa na utaonekana kuwa na mvuto kwa
watu wengine na hasa pale utakapokutana na mtu Special kwako.
Kumbuka kwamba hisia za mwanzo mara nyingi huwa sio zakuaminika, hasa
unapokuja katika swala la kutongozana katika mitandao mbali mbali ya
Internet, watu huwa hawaweki uhalisia wao mbele, bila kujali mmekutana
wapi, lini, kivipi, chamsingi kabla ya kuwa karibu sana na mtu, nivyema
ukawa naye katika hali mbali mbali kama vile, wakati wa shida na raha.
Kwamfano utampima mtujinsi alivyokuchukulia wakati wa matatizo na wakati
wa raha.
Kuwa mkweli na muwazi, jivunie ulichonacho, usitake
mtu akupende kwa ndoto zako au matarajio kuwa mtu flani baadaye.
Kwamfano unamwambia mpenzi wako kuwa baada ya mwaka moja nitanunua gari,
au nitapata kazi au nitakuwa msanii. Inapaswa kupendwa vile ulivyo kwa
wakati huo.
Kikubwa zaidi, wekeza kwanza katika mahusiano imara
na sio kukimbilia kufanya mapenzi. Japokuwa katika zama hizi za kizazi
cha sasa ni vigumu mtu kuchukua muda wa kumfahamu mtu kwanza. Unapaswa
kuwa na mtu kwa takribani muda kadhaa ili mfahamu kama mnaendana kitabia
au lah!.