BINTI AJINYONGA BAADA YA UGOMVI WA CHAPATI

7 years ago97 Views

Binti wa miaka 20, ajulikanaye kama Sharon, mkazi wa Kisumu, Kenya, amejinyonga hadi kufa baada ya majibizano baina yake na shangazi yake kuhusu chapati.


Inaelezwa kuwa Sharon aliachiwa fedha kwa ajili ya kununua chakula na kupika kwa ajili ya familia na badala yake alinunua chapati cha maharage na kula mwenyewe.

Kwa mujibu wa jirani wa familia hiyo, Jane Auma, shangazi yake aliporudi nyumbani na kuuliza kwanini binti huyo hakupika chakula cha familia nzima na badalayake akajinunulia chapati, wawili hao walianza kujibiza na baadaye, msichana huyo aliamua kujiua kwa kujinyonga.

Auma anasema ni ngumu kuamini kuwa msichana huyo angeweza kujinyonga kwa mzozo wa chapati, lakini hatahivyo ujumbe wa alioacha ameuandika tayari umefikishwa polisi.

Mwili wa marehemu umeshapelekwa kuhifadhiwa kwenye hospitali ya Jaramogi Oginga na upelelezi unaendelea. 

from MALUNDE 1 BLOG https://ift.tt/2J2zBS0
via

0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.