ATOLEWA NJE YA NDEGE BAADA YA KUNASWA AKIOMBA ‘MUNGU WAKE’ WAPATE AJALI ANGANI

7 years ago87 Views

Mwanaume mmoja ametolewa kutoka kwenye ndege moja iliyokuwa ikisafiri kutoka Uwanja wa Ndege wa Islamabad nchini Pakistan kwenda Dubai, baada ya kufanya maombi akimuomba ‘mungu wake’ kusababisha ajali ya ndege hiyo.

Abiria huyo ambaye alitambuliwa kwa jina moja la Khalil alikuwa akisafiri kuelekea Australia kupitia Dubai, na imefahamika kuwa alianza kuomba maafa ya mauti yatokee punde tu alipoketi ndani ya ndege hiyo katika Uwanja wa Ndege.

Maombi yake yaliwafanya abiria kuhofia na kuanza kuingiwa na wasiwasi, hasa wasafiri na wahudumu wa ndege waliokuwapo.

Baada ya tukio hilo Rubani alitahadharisha idara ya ulinzi katika uwanja huo , na maafisa wa usalama walipofika wakamuondoa ndani ya ndege.
Chanzo – Daily Mail UK

from MALUNDE 1 BLOG https://ift.tt/2HevqAH
via

0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.