Wasira: Chadema Wapo Honeymoon, Wanaenda Kujifungia Mahala”

Admin Updates4 months ago54 Views

 Wasira: Chadema Wapo Honeymoon, Wanaenda Kujifungia Mahala"

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amesema Chama na Serikali yake hawatokubaliana na azimio lolote litakalotolewa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) baada ya kukutana kwa faragha kama walivyotangaza Viongozi wa Chama hicho juzi.

Wasira amesema baada ya kusikia kuwa Chama hicho kimetangaza kuwa kinakwenda kujifungia kisha kije na jambo ambalo halijapata kushuhudiwa Nchini, ametoa angalizo kuwa jambo hilo ni lazima lifuate sharia za Nchi.

Wasira amesema haya leo alipohutubia Wananchi katika mkutano uliotumika kuzindua sherehe za maadhimisho ya miaka 48 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi uliofanyika katika uwanja wa Stendi ya zamani mjini Bunda.

“Wamesema wanajifungia halafu waje wafanye jambo ambalo halijapata kuonekana, nikasema ni jambo gani, mimi nikaona huko kujifungia ile ni honeymoon maana honeymoon simnaijua, Watu wakishaoana wanajifungia mahali…ile ni honemoon”

“Tunawaambia tunawatakia heri kwenye honeymoon lakini tunawaambia lolote watakalotoka nalo kwenye honeymoon lazima lifuate sheria, wakija na honeymoon inavunja amani hatuwezi kuwaunga mkono” ——— Wasira.

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.