
“Sisi tumeamua wote kwa pamoja tunajiondoa Chadema ili tuwaachie hicho chama waendeshe wanavyotaka kwasababu sisi hatuwezi kuwa sehemu, hatuwezi kuwa wanachama wa Chama ambacho maamuzi yake hayafanywi kwa vikao, hatuwezi kuwa wanachama wa chama ambacho wanachama wanabaguliwa, hatuwezi kuwa wanachama wa chama ambacho Katiba haifuatwi. Hatuwezi kuwa wanachama wa namna hiyo kwasababu sisi sio chawa, sisi ni Viongozi, sisi tunajitambua na tuliingia Chadema kwasababu ya malengo na tunatoka Chadema kwasababu Chadema imeachana na malengo yaliyotufanya tuingie.
Kwa hiyo tunajitoa Chadema ili wasipate sababu kwamba Chama hiki kilikufa kwasababu walikuwepo. Na ili nisiwaachie maswali mtu anaweza akauliza sasa tunaenda wapi, sisi sio wazee wa kufikia umri wa kustaafu. Tutaendelea kuwapigania watanzania na tutatafuta jukwaa muafaka.”-Benson Kigaila, Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) bara akizungumza wakati wa mkutano na wanahabari uliofanyika kati ya waliokuwa Wajumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA taifa mpaka tarehe 22 Januari 2025, na wanahabari mkoani Dar es Salaam siku ya Jumatano.