UNAJUA Kwanini Mapenzi ya Mbali Hayadumu? Hizi Hapa Sababu 5..!!!

Special Correspondent6 years ago7 Views

Wengi wetu hujiuliza kwanini  maisha ya mapenzi ya mbali huwa  hayafiki mbali na kubaki wa kijiuliza tatizo ni nini? Wakati mwingine watu huanza kuulizanaa mchawi ni nani katika mapenzi yao. Laa hasha!! Huenda mchawi wa mapenzi yako ni wewe mwenyewe lakini hujui kwa sababu hakuna mtu ambaye ameshawahi kukueleza jambo hili na lile ndio tatizo

Hata hivyo hakuna kumbukumbu ambazo zinaonesha ni kwa asilimia ngapi ambazo wapenzi wanapenda kuwa mbali mbali japo mazingira mara nyingi ndo huwa chanzo


Katika tafiti mbali mbali zinaonesha kwamba umbali humaliza kabisa mapenzi ambayo  wapenzi wengi wenye malengo ya kufika mbali huwakuta.


Lakini zipo sababu mbalimbali ambazo ukizichanganua utajua kwa nini mapenzi mengi ya mbali huw hayadumu


Wivu.


Wivu huwa ni chachu ya kupima upendo lakini ukizidi pia huwa tatizo. Wivu wa mapenzi  ukizidi husababisha kutokuaminiana  kwani kila mmoja kwa wakati wake tofauti huhisi mwenzake anamsaliti, mara nyingi hali kama hii humfanya mmoja wapo kati ya wapenzi hao wawili kuona kama mwenzake ameshamchoka na anamtafutia sababu. Ni vyema kuwa na wivu kiasi kwa mpenzi wako


Mawasiliano


Mawasiliano huimarisha mapenzi na hufanya wahusika kujihisi wapo pamoja. Inapotokea kuwa na ufinyu wa mawasiliano ndipo hali ya mapenzi ya upande mmoja hupungua na kuhisi kwamba tayari mwanamke/mwanaume tayari ameshapata mwingine wakumfanya asifanye mawasiliano ya mara kwa mara.


Ugomvi


Magomvi ya mara kwa mara hufanya mmoja wenu ahisi kuchoka na mahusiano. Inapotokea sababu za  ugomvi ambao unahisi unaweza kuwa chanzo cha kuvunja mahusiano yenu ni afadhali ukazizuia na kutafuta siku nyingine ya kutatua tatizo hilo.


Kutojali


Hii mara nyingi imetajwa sana kuwa ni chanzo cha mapenzi ya mbali kuvunjika kwa sababu  tofauti mfano mpenzi wako alipokuwa karibu ulikuwa ukimpatia huduma mbalimbali kama zawadi nk, lakini anapokuwa mbali unajisahau hali hii humfanya mpenzi wako ajiulize kulikoni?


Usikivu


Nayo ni sababu ambayo ukiwauliza wengi wao ambao walikuwa na uhisiano wa mbali ukavunjika lazima atakulalamikia kwamba alikuwa hanisikilizi nachomwambia. Mfano alitaka kutoka kwenda ‘OUT’ na wenzake nikamyima lakini hajanisikiza hivyo hanifai.


Hizi huenda zikawa ni baadhi ya sababu ambazo wapenzi wengi ambao mapenzi yao hayajafanikiwa kama jinsi walivyo hitaji wamekumbana nazo.


Ili kuepuka changamoto za kutengana  na mtu ambaye unamuhitaji katika maisha yako ni vyema ukaanza kujifunza pole pole kutoka kwake ili siku ukiwa mbali naye ujue kipi mwenzako anapenda na kipi hakipendi mnapokuwa mbali.


Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.